Friday, October 25, 2013

AUNT LULU ATANGAZA KUACHA KUJIUZA.....

Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’

MWANADADA Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’ ameibuka na kusema kuwa sasa hawezi kurudia biashara ya kujiuza na kuwataka wanaodhani kuwa bado yuko na tabia hiyo waondoe hisia hizo kwani kwa sasa si Lulu wa zamani tena.

Akizungumza  hivi karibuni, Anti Lulu alisema sasa hivi amejipanga kuyaendesha maisha yake kihalali na kwa kiasi kikubwa amefanikiwa licha ya kuwepo kwa baadhi ya watu wanaotaka kumrudisha nyuma.
“Watu wameniibia dukani kwangu ili kunirudisha nyuma lakini wamenoa, sirudii zama za kujiuza tena. Duka nimeshalijaza, nimenunua kiwanja huko Bunju na muda si mrefu nitaanza kujenga.
“Niwashukuru sana waandishi wa habari kwa kunibadili tabia kwani huenda mpaka leo ningekuwa nafanya mambo ambayo hayana tija kwenye jamii,” alisema Anti Lulu.

SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.

0 comments em “AUNT LULU ATANGAZA KUACHA KUJIUZA.....”

Post a Comment

 

FULL MAUDAKU Copyright © 2011 -- Template created by MAMBOMSETO TEAM -- Powered by MAMBOMSETO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter