Friday, October 25, 2013

DUDE NDANI YA KASHFA YA KUTOKA KIMAPENZI NA KIMADA WA MUHESHIMIWA MBUNGE

Kulwa Kikumba ‘Dude’.
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kiko karibu na msanii huyo, mbunge huyo kwa sasa ameshagundua kuwa Dude ana uhusiano na ‘nyumba ndogo yake’ hiyo.
Taarifa hizo zilizidi kudai kuwa, hapo awali mheshimiwa huyo ‘hakukausha nyayo’ kwa mrembo huyo lakini baada ya kugundua hali ya ‘sintofahamu’ baina ya Fetty na Dude, amesitisha ukaribu na mrembo huyo.
Baada ya kutonywa habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Dude ili kujua ukweli wa mambo, alipopatikana alisema:
“Ni kweli hata mimi hizo habari nimezisikia kutoka kwa wasanii wenzangu na zinaniumiza sana kwani mimi najua Fetty ana bwana wake tena mheshimiwa.

Naogopa sana kutekwa, naomba kupitia gazeti hili huyo mheshimiwa aelewe kwamba mimi sina uhusiano mbaya na mwanamke wake, tumefahamiana kupitia filamu tu,” alisema Dude.
Fetty alipotafutwa kwa njia ya simu,  iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.

0 comments em “DUDE NDANI YA KASHFA YA KUTOKA KIMAPENZI NA KIMADA WA MUHESHIMIWA MBUNGE ”

Post a Comment

 

FULL MAUDAKU Copyright © 2011 -- Template created by MAMBOMSETO TEAM -- Powered by MAMBOMSETO TEAM

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter