Injini na Mabehewa ya reli hiyo kongwe Tanzania vimechakaa wakati ni tegemeo kubwa kwa wakazi wengi wa baadhi ya mikoa ya Tanzania na pia ni sehemu nyingine ya kuukuza uchumi wa nchi.
Rais wa kampuni hii ya China amemwambia Waziri mkuu kwamba tayari wameanza mazungumzo na Wizara ya uchukuzi na kama watakubaliana, wako tayari kuja Tanzania na kuijenga hii reli ikiwa ni kampuni ambayo pia iliijenga reli ya Tazara baada ya Hayati Mwalimu Nyerere kuiomba serikali ya China.
Waziri mkuu Mizengo Pinda alisema kuna kampuni kadhaa kutoka mataifa mbalimbali ambazo zimeonyesha nia ya kujenga reli hiyo lakini waliona wawasiliane na China kwanza ambayo kuna historia ya ushirikiano mzuri.
Kutokana na uchakavu wa hii reli ya kati, kiwango cha kusafirisha mizigo ya ndani na nje ya nchi kimeshuka ambapo siku za safari za treni ya abiria zimeshuka kutoka safari saba kwa wiki mpaka safari mbili kati ya Dar es salaam, Mwanza na Kigoma.
SHARE HABARI HII KWA RAFIKI ZAKO HAPA CHINI==>>
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU BASI BOFYA "LIKE" HAPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK.